Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Mei 04, 2025 Local time: 23:42

Serikali ya mpito ya Syria yafikia makubaliano ya amani na Wakurdi


Rais wa mpito wa Syria Ahmed al-Sharaa na kamanda wa waasi wa Kikurdi Mazloum Abdi, baada ya kusaini makubaliano ya amani, Machi 10, 2025.
Rais wa mpito wa Syria Ahmed al-Sharaa na kamanda wa waasi wa Kikurdi Mazloum Abdi, baada ya kusaini makubaliano ya amani, Machi 10, 2025.

Serikali kuu ya Syria imefikia makubaliano na mamlaka inayoongozwa na Wakurdi ambao wanadhibiti eneo la kaskazini mashariki mwa nchi, ikiwa ni pamoja na sitisho la mapigano na kushirikishwa katika jeshi la Syria kwa kundi hilo linaloungwa mkono na Marekani.

Makubaliano hayo yalisainiwa Jumatatu na Rais wa mpito Ahmad al-sharaa na Mazloum Abdi, Kamanda wa kundi la waasi wa Kikurdi wanaoungwa mkono na Marekani.

Makubaliano hayo yanaashiria mafanikio makubwa ambayo yataiweka sehemu kubwa ya Syria chini ya udhibiti wa serikali inayoongozwa na kundi lililoongoza uasi wa kumuondoa madarakani Rais Bashar Assad mwezi Disemba.

Makubaliano hayo yatakayotekelezwa mwishoni mwa mwaka huu yatarejesha maeneo yote ya mpaka na Iraq na Uturuki huko kaskazini mashariki, viwanja vya ndege na maeneo ya mafuta chini ya udhibiti wa serikali kuu.

Wakurdi watapewa tena haki zao ikiwemo kufundisha na kuzungumza lugha yao, haki ambazo zilikuwa zimepigwa marufuku kwa miongo kadhaa chini ya utawala wa Assad.

Forum

XS
SM
MD
LG