Rais wa zamani wa Marekani atarajiwa kufikishwa mahakamani kufunguliwa mashtaka

Your browser doesn’t support HTML5

Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kukamatwa rasmi na kufikishwa mahakamani Jumanne, ikiwa mara ya kwanza kwa kiongozi wa zamani wa White House kukabiliwa na mashtaka ya uhalifu.

Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kukamatwa rasmi na kufikishwa mahakamani Jumanne, ikiwa mara ya kwanza kwa kiongozi wa zamani wa White House kukabiliwa na mashtaka ya uhalifu.

Katika hatua isiyo ya kawaida ya historia ya Marekani, jopo la mahakama huko New York lilipiga kura Alhamisi iliyopita kumshtaki Trump kwa mashtaka yanayohusiana na kumlipa mcheza filamu za ngono wakati wa kampeni yake ya urais 2016.

Matangazo ya Duniani Leo kutoka idhaa ya kiswahili ya Sauti Amerika, Washington, D.C.
#habari