Shambulizi la kombora la Russia lilipiga mji wa kati wa Ukraine wa Kryvyi Rih na kuuwa afisa wa polisi na kujeruhi darzeni wengine, Waziri wa Mambo ya Ndani Ihor Klymenko alisema. Kryvyi Rih ni mji aliozaliwa Rais wa Ukraine Volodomyr Zelenskyy.
Wakati huo huo, jeshi la anga la Ukraine lilitungua ndege zisizo na rubani 16 kati ya 20 za Shahed zilizotengenezwa Iran katika eneo la Odesa la Ukraine zilizorushwa kutoka Russia mapema Ijumaa kulingana na maafisa wa kijeshi.
Hii ilikuwa mara ya tano wiki hii Odesa kulengwa, gavana wa mkoa Oleh Kiper alisema kwenye programu ya ujumbe wa Telegram..
Katika shambulio lingine, takriban watu watatu walijeruhiwa baada ya mgomo wa Russia katika mji wa Sumy kaskazini mashariki mwa Ukraine.
Zelenskyy alivipongeza vikosi vitatu vya kijeshi Alhamisi kwa hatua aliyoiita sahihi dhidi ya wanajeshi wa Russia walioko mashariki na kusini mwa Ukraine kama sehemu ya uvamizi unaoendelea wa Kyiv.
Kikosi kimoja cha walinzi wa kitaifa kilikuwa kikipigana upande wa mashariki na viwili kusini, Zelenskyy alisema katika hotuba yake ya usiku kwa njia ya video.