Kennes Bwire is a journalist with Voice of America and is based in Washington DC.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekutana na rais wa China Xi Jinping mjini Beijing na kusaini mikataba mbalimbali ya ushirikiano ambayo wanadiplomasia wamesema itanufaisha kila upande.
Jeshi la Kenya KDF, linatayarisha kikosi chake kukituma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kama sehemu ya kikosi cha Jumuiya ya Afrika Mashariki kupambana na makundi ya waasi ambayo yamepelekea kukosekana kwa amani sehemu hiyo.
Marekani imeshumu mapigano yanayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kati ya kundi la waasi la M23 na wanajeshi wa serikali ya DRC na kuwataka waasi kuachilia sehemu wanazozishikilia na kuweka chini silaha.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema kwamba haitafanya mazungumzo na kundi la waasi la M23, ikilitaja kundi hilo ni la kigaidi.
Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imemuita balozi wake wa Rwanda kurudi Kinshasa kwa mashauriano.
Rwanda imetuma wanajeshi kwenye mpaka wake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, saa chache baada ya DRC kumfukuza balozi wa Rwanda kwa madai ya DRC kwamba serikali ya rais Paul Kagame inawaunga mkono waasi wa M23.
Rais wa Kenya Dr. William Ruto, amesema kwamba yupo tayari kufanya kazi na mmoja wa viogogo wa muungano wa Azimio Kalonzo Musyoka.
Mshauri wa usalama wa taifa wa rais wa Marekani Jake Sullivan, amefanya mazungumzo na mwenzake wa Kenya Dr. Monica Juma kuhusu vita vya Ethiopia na mgogoro wa kibinadamu unaoendelea kuongezeka nchini humo.
Mfuasi mkubwa wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda Sam Mugumya, ambaye amekuwa akizuiliwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa muda wa miaka 8, ameachiliwa huru.
Waziri Mkuu wa Uingereza Liz Truss amejiuzulu kama kiongozi wa chama cha Conservative.
Mshauri wa ngazi ya juu kuhusu operesheni maalum wa rais wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amesema kwamba hataacha kuandika ujumbe wenye utata kwenye mitandao ya kijamii na kwamba yeye si mtoto wa kuambiwa cha kufanya.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema haitafanya mazungumzo na kundi la waasi la M23, baada ya kundi hilo kusema kwamba lipo tayari kwa mazungumzo hayo.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesaini mswaada wa matumizi ya mitandao ya kijamii na kuwa sheria na hivyo kuwaweka watumiaji wa mitandao hiyo katika hatari ya kufungwa hadi miaka 5 gerezani endapo watachapisha au kusambaza haabri ambazo zinaikera serikali au watu binafsi.
Idadi kubwa ya nchi wanachama katika Umoja wa Mataifa zimepiga kura ya kuikashifu hatua ya Russia kwa kujiingiza katika mikoa minne ya Ukraine.
Mgombea wa urais mara 5 bila mafanikio nchini Kenya Raila Odinga, ameendelea kuishutumu mahakama na tume ya uchaguzi, akidai kwamba alipokonywa ushindi katika uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti.
Aliyekuwa kiongozi wa walio wengi katika bunge la taifa wakati wa utawala wa rais mstaafu Uhuru Kenyatta, Amos Kimunya, amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya ufisadi.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ammueahidi rais wa Somalia kwamba Uganda itaendelea kutoa msaada wa sialaha kwa nchi hiyo ili kupambana na wanamgambo wa Al-shabaab, lakini nchi hiyo inastahili kujijenga yenyewe kiusalama.
Mgombea wa urais mara tano nchini Kenya bila mafanikio Raila Odinga, amedai kwamba alipoteza uchaguzi wa mwezi Agosti mwaka huu kwa sababu nchi za nje ziliingilia uchaguzi huo na kwamba zilimpendelea mpinzani wake.
Watu 29 wamefariki kutokana na mlipuko wa virusi vya Ebola nchini Uganda. Maafisa wa afya 4 ni miongoni mwa waliofariki.
Mahakama kuu nchini Kenya imemhukumu mbunge miaka 67 gerezani baada ya kupatikana na makosa ya ufisadi.
Pandisha zaidi