Mamlaka za Nigeria zimesema Jumatatu kuwa wafungwa 281 wametoroka baada ya mafuriko kuangusha kuta za jela kaskazini mashariki mwa nchi.
Kenya imetoa kadarasi ya usambazaji wa umeme kupitia ushirikiano na sekta ya kibinafsi na kampuni ya Adani ya India, pamoja na benki ya Maendeleo ya Afrika, kulingana na mshauri mkuu wa kiuchumi wa rais, David Ndii.
Ukraine Alhamisi iliishtumu Russia kwa kutumia makombora ya kimkakati kushambulia meli ya nafaka ya kiraia katika shambulizi la kombora katika bahari ya Black Sea karibu na Romania, nchi mwanachama wa NATO, na kuzidisha mvutano kati ya Moscow na muungano huo wa ushirika wa kijeshi.
Marekani inaunga mkono hatua ya kuongeza viti viwili vya kudumu kwenye baraza la usalama la umoja wa mataifa kwa ajili ya mataifa ya Afrika.
Kundi la wanamgambo la Hamas Jumatano lilisema kwamba wapatanishi wake wamesisitiza utayari wake wa kutekeleza sitisho la vita la “mara moja” na Israel huko Gaza, kulingana na pendekezo la hapo awali la Marekani bila masharti ya kutoka upande wowote.
Mahakama ya Juu ya Kenya imesitisha kwa muda mkataba wa kukodishwa kuwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta – JKIA, kwa muda wa miaka 30, kwa kampuni ya India ya Andani Group, kwa lengo la kuupanua.
Aliyekuwa mpenzi wa mwanariadha wa Uganda Rebecca Cheptegei, anayedaiwa kumuuwa kwa kumchoma baada ya kummwagia petroli, ameripotiwa kufariki pia, kutokana na majeraha ya moto aliyopata wakati wa tukio hilo.
Rais wa Algeria Abdulmadjid Tebboune ameshinda uchaguzi wa urais nchini Algeria na ushindi wake kuangaziwa zaidi na vyombo vya habari nchini humo.
Mgombea wa upinzani kwenye uchaguzi wa rais nchini Venezuela Edmundo Gonzalez alisafiri kuelekea Uhispania kuomba hifadhi, Madrid imesema.
China Jumapili ilisema itaruhusu kuanzishwa kwa hospitali zinazomilikiwa na wageni katika maeneo tisa ya nchi ikiwemo mji mkuu, huku Beijing ikijaribu kuvutia zaidi uwekezaji wa kigeni ili kukuza uchumi wake unaosusua.
Takriban watu 48 walifariki Jumapili katika mlipuko wa lori la kubeba mafuta baada ya kugongana na gari nyingine katika jimbo la Niger lililo eneo la kati, la kaskazini mwa Nigeria, idara ya kusimamia majanga katika jimbo hilo imesema.
Mkutano wa nane kati ya China na wafanyabiashara kutoka Afrika umeanza hii leo Ijumaa mjini Beijing, China, ikiwa ni sehemu ya mkutano mkuu unaonendelea kati ya viongozi wa Afrika na China.
China, Tanzania na Zambia zimesaini makubaliano ya kukarabati reli iliyojengwa miongo kadhaa iliyopita kwa lengo la kuboresha usafiri wa mizigo kwa kutumia njia ya reli na bahari kati nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
Kamala Harris ameahidi kuchukua msimamo mkali juu ya uhamiaji katika eneo la mpaka wa kusini wa Marekani na kusema hatozuia upelekaji silaha kwa Israel.
Mkuu wa sera ya kigeni katika Umoja wa Ulaya Josep Borrel Alhamisi alisema aliziomba nchi wanachama kutafakari uwezekano wa kuwawekea vikwazo mawaziri wawili wa Israel kwa “ matamshi ya chuki” dhidi ya Wapalestina, matamshi ambayo amesema yanakiuka sheria ya kimataifa.
Jaji mmoja wa Ufaransa Jumatano alimuweka mmliki wa mtandao wa Telegram Pavel Durov chini ya uchunguzi rasmi dhidi ya uhalifu uliopangwa kwenye app hiyo ya kutuma ujumbe.
Baadhi ya sehemu za mashariki mwa Sudan zimekumbwa na mafuriko baada ya bwawa kuvunjika na kuharibu vijiji 20 na kusababisha vifo vya watu 30.
Waendesha mashtaka wa Ufaransa Jumatatu walisema Pavel Durov, mwanzilishi wa mtandao wa Telegram na mzaliwa wa Russia, alikamatwa nchini Ufaransa kama sehemu ya uchunguzi kuhusu uhalifu unaohusiana na kushirikisha watoto katika tendo la ngono, na miamala ya ulaghai kwenye mtandao huo.
Wakati mazungumzo muhimu ya Somalia yakipangwa kuanza Jumatatu mjini Ankara, Uturuki, waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amesema kuwa wanatafuta jinsi ya kufikia bandari kwa njia ya mashauriano.
Polisi wa Uganda wamesema Jumapili kuwa idadi ya vifo kutokana na maporomoko ya ardhi kwenye eneo kubwa la kutupia taka mjini Kampala imefikia 13, wakati timu za uokozi zikiendelea kutafuta manusura.
Pandisha zaidi