Milipuko mikubwa na milio ya risasi ilitikisa sehemu za mji mkuu wa Sudan, Khartoum na mji pacha wa Omdurman mapema ijumaa, wakaazi wamesema. Hili linajiri licha ya kuongezwa muda wa sitisho tete la mapigano kati ya majenerali wakuu wawili ambao mzozo wao wa kugombea madaraka umeuwa mamia ya watu.
Matangazo ya Duniani Leo kutoka idhaa ya kiswahili ya Sauti Amerika, Washington, D.C.
#habari