Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman, na Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, Jumanne wamekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji, huku wakitoa wito wa sitisho la mapigano huko Gaza na Lebanon, wakati wa mazungumzo yao mjini Cairo.
Wakaazi wa mji mkuu wa Lebanon Beirut Jumanne wameendelea kuwa na wasiwasi baada ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kutishia kuendelea na mashambulizi dhidi ya Hezbollah kote Lebanon pamoja na mji mkuu.
Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gashagua atakabiliana na Seneti katika kesi ya kutaka kuondolewa madarakani, baada ya mahakama ya juu mjini Nairobi, Kenya kukataa kutoa maagizo ya kuizuia Seneti kuendelea na mjadala.
Wizara ya Afya ya Zimbabwe Jumapili imethibitisha kesi mbili za kwanza za maambukizi ya mpox bila kueleza kwa kina aina kamili ya virusi hivyo.
Ofisi ya rais wa Afrika Kusini imesema Jumapili kwamba waziri wa zamani wa Fedha na Kazi ambaye pia alikuwa gavana wa kwanza mweusi wa Benki Kuu, Tito Mboweni, ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 65 baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Rais wa Marekani Joe Biden na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu walizungumza Jumatano kuhusu mpango wa Israel wa kulipiza kisasi dhidi ya Iran, huku kundi la Hezbollah likisema wapiganaji wake waliwarudisha nyuma wanajeshi wa Israel kwenye eneo la mpakani.
Kampuni ya TikTok inakabiliwa na kesi mpya zilizowasilishwa Jumanne na majimbo 13 ya Marekani na jimbo la District of Columbia, yakiushtumu mtandao huo wa kijamii maarufu, kwa kudhuru na kushindwa kulinda vijana.
Kimbunga Milton kinaelekea Pwani ya Ghuba ya Florida, hapa Marekani, na kufikia dhoruba ya kiwango cha tano Jumanne, na kusababisha msongomano mkubwa wa magari na uhaba wa mafuta, huku maafisa wakiamuru zaidi ya watu milioni 1 kukimbia kabla hakijakumba eneo la Tampa Bay.
Meli yenye bendera ya Palau ilishambuliwa Jumatatu na kombora la Russia katika bandari ya kusini mwa Ukraine ya Odesa, kombora hilo liliua raia mmoja wa Ukraine na kujeruhi wahudumu watano katika shambulizi la pili kama hilo katika kipindi cha siku kadhaa, maafisa walisema.
Papa Francis atawateuwa makadinali wapya 21 kutoka duniani kote, alisema hayo Jumapili, katika hatua ambayo haikutarajiwa kushawishi kundi hilo lenye nguvu la watu wa kanisa ambao siku moja watamchagua mrithi wake.
Waziri mkuu wa Haiti Garry Conille alianza ziara huko Umoja wa Falme za Kiarabu na Kenya mwishoni mwa juma kutafuta msaada wa usalama, baada ya moja ya mashambulizi mabaya ya magenge ambayo nchi hiyo haijawahi kushuhudia katika miaka ya hivi karibuni.
Mwenyekiti wa kampuni ya mafuta ya Total Energies, Patrick Pouyanne ambaye pia ni mkurugenzi mkuu amesema Jumatano kwamba anapanga kuzuru Msumbiji baadaye mwezi huu kwa ajili ya mpango wa kuwekeza nchini humo.
Washika dau wakuu kwenye Shirika la Kimataifa la Fedha, IMF, wamesihi Kenya itoe ombi kwa IMF la kuchunguza madai ya ufisadi na utalawa mbaya, kama hatua kuelekea kupata mikopo iliyokwama kufuatia kusitishwa kwa mswada wa fedha uliolenga kuongeza kodi.
Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris Alhamisi aliahidi msaada kwa Ukraine, akimuzungumzia mpinzani wake Donald Trump bila kumtaja jina, akisema wale ambao wanataka Ukraine ibadilishe ardhi yake kwa ajili ya amani na Russia, wanaunga mkono “mapendekezo ya kujisalimisha.”
Jeshi la Sudan limefanya mashambulizi ya mizinga na ya anga katika mji mkuu wa Sudan Alhamisi katika operesheni kubwa sana ya kukomboa tena maeneo ya huko tangu vita vyake vya miezi 17 kuzuka na vikosi vya RSF , mashahidi na vyanzo vya jeshi vimesema.
Ibada ya kumbukumbu imefanyika leo Alhamisi kwa ajili ya wavulana 21 waliofariki katika ajali ya moto kwenye shule mapema mwezi huu.
Benki ya dunia Jumatatu ilisema kwamba Denmark imeahidi kutoa mchango wa dola milioni 491.7 kwa mfuko wa benki hiyo ili kusaidia nchi maskini, likiwa ongezeko la asilimia 40 ikilinganishwa na mchango wa awali wa nchi hiyo.
Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump amesema hatawania muhula wa nne mfululizo wa urais ikiwa atashindwa kwenye uchaguzi wa tarehe 5 Novemba, akisema hayo katika mahojiano yaliyochapishwa Jumapili.
Kikosi cha mapinduzi cha Iran Jumapili kilisema kiliwakamata watu 12 kwa kuwa majasusi wanaoshirikiana na Israel ambao walikuwa wanapanga vitendo vya kuvuruga usalama wa Iran.
Ofisi ya rais wa Nigeria imesema Alhamisi kwamba kampuni ya Coca Cola inapanga kuwekeza dola bilioni moja kwenye operesheni zake nchini humo ndani ya miaka mitano ijayo kufuatia mkutano kati ya wakurugenzi wake na Rais Bola Tinubu.
Pandisha zaidi