Mchezaji huyo wa hali ya juu alikuwa akitibiwa saratani ya utumbo mpana tangu 2021. Alikuwa amelazwa hospitali mwezi uliopita akiwa na maradhi mengi. Aliibeba Brazil hadi kwenye kilele cha soka na kuwa balozi wa kimataifa wa mchezo huo katika safari iliyoanzia mitaa ya jimbo la Sao Paulo, ambapo alicheza mpira wa kutengenezwa na soksi iliyojaa magazeti au matambara. Gwiji huyo wa Brazil, ambaye jina lake halisi lilikuwa Edson Arantes do Nascimento, aliisaidia nchi yake kushinda Kombe la Dunia mwaka wa 1958, 1962 na 1970 na anabakia kuwa kinara wa ufungaji wa timu ya taifa akiwa amefunga mabao 77 katika mechi 92 #pele #mfalmewasoka #brazil #ugonjwa #saratani #kombeladunia #bingwa #voa #voaswahili #dunianileo
Matukio
-
Machi 14, 2025Changamoto za ulezi wa watoto walemavu kiakili Kenya
-
Februari 28, 2025Waislamu wajitayarish kwa Ramadhani
-
Februari 27, 2025Ethiopia na Somalia waimarisha uhusiano wao
-
Februari 18, 2025Nini kilichosababisha Raila Odinga kushindwa katika uchaguzi wa AU?
-
Februari 11, 2025Naibu Katibu Mkuu aeleza hatua za dharura zinazochukuliwa DRC